Ticker

6/recent/ticker-posts

ZIFAHAMU ROHO SABA ZA MUNGU

 Roho Saba za Mungu
Image result for keith miller seven spirits god


Utangulizi

Nambari saba lilisikiliwa kuwa takatifu kati ya taifa la Kisemiti na yaonekana kuenezwa tokea Nuhu hadi mataifa yote, Wamisiri waliesabu nne kuwa takatifu lakini hata kwenye mfumo wao saba pole pole ilitwaa mahali pa nne. Nambari saba ilibantilishwa pole pole chini ya mfuno wa kishenzi na katika Shamani na ikawa miungu saba ya mipao ya nguzo za ulimwengu au muhimili wa mundi (Taz. Sura hii  Kujitolea na kutafakari sana habari za Mungu sura ya 1. Kutangaza siri za Wababuloni (B7 11).



Umuhimu wa saba kama tarehe za dini za siku ya saba tokea karne ya ishirini na tatu kabla ya kucha kwa Masihi (BCE) katika  kumbukumbu za cuneiform (Taz. Kamusi ya kutafsiri Biblia, vol. 3werevu. ‘saba’, kadha wa kadha;  somo sare, Abingdon, 1980). Kivingine mwanzo wake ulikuwa wakati wa Nuhu.



Hivyo sherehe za siku ya sabaya Biblia zimetambulika zikiendelea pale Mesopotamia tangia wakati wa Nuhu. Hapo sheria za Musa zilifanya kazi tokea Nuhu na chini ya sham, Kristo pia alitia nguvu zile sheria alizotoa kwa adamu na wazee wa imani na zilizotekelewza na kwendelezwa na Nuhu hadi baada ya gharika.



Sherehe za tarumbeta, upatanisho na za vipanda pia zilitekezwa katika mwezi wa saba na kuashiria utimisho katika sura  za mpango wa Mungu vile inavyofunuliwa katika takuimu takatifu.



Sherehe za majuma au siku ya roho, (kumb. 16:9) na sherehe za sikukuu (Lawi 25:8-10) zote zimeasiliwa  tokana na mraba wa saba jinsi ilivyokuwa katika Hekalu lenyewe, kuambatana na mlolongo wa tano kuwakilisha patakatufu pa patakatifu vyote kama Hekalu onekanefu na Hekalu la kiroho ambayo ni kanisa la Mungu.



Asili ya Juma la siku sabailitokana kwenye uzao wa Nuhu pale Mesopotamia na ilionekana katika elimu ya dini na elimu ya kidunia ya kisumeria na kiakaddia (ibid). Ilifikiriwa na kuaminika kwamba sayare saba  zilivyo tajwa pia , zilitekeleza sehemu fulani katika utakatifu wa idadi hiyo, walakini inaweza kuaminika kwa urahisi kwamba hii ilikisiwa kutia umuhimu katika mfumo wa kisayari kama   ushuhuda wa sehemu ya Mungu katika uumbaji. Kudhoofika kwa muundo wa kidini ulitokea Babuloni na tunajua kwamba ilitendeka katika kipindi cha baada ya gharika cha Nuhu na mwanawe shem.



Mwezi mwandamo na juma ya siku saba vimekubalika kuwa mifumo inayojitengemea na juma haikutokea toka mwezi mwandamo  kabisa (ibid).



Kutokana naushahidi tulio nao inaonekana juma ilianzihswa tokea sura ya kwanza ya mfumo wa baada ya gharika katika wakati wa Nuhu.



Nambari saba na muundo wa saba na sabini ulikuwa na umuhimu wa kiroho.



Nambari saba huwa na umuhimu katika elimu ya dini ya Agano la Kale kuwa ufafanuzi wake ni upana na umehusishwa.



Kwa kweli inakafakariwa kuwa ni vigumu kutenganisha matumishi ya saba kutokana na maana halisi ya kiroho hili kubainisha wakati itatumika hivi tu kuashiria nambari maalumu.



Saba na mifumo yake imetumuika katika mchakato wa utakazo wa ukuhani na katika  kubariki  matabahu. (Kutoka 29:35-37), kafara kawida huwa katika vikundi vya saba. Kwa kweli zimekuwa sehemu kama jozi takatifu ya mnyama kutoka mwanzo chini ya Nuhu, mchakato wa kutoa kafara uhusisha saba katika utaratibu wa ibada. (Mwanzo 7:2-3; 8:20); 21:28–30; Hesabu 28:11; 1Mambo ya nyakati 15:26; Ayubu 42:8). Kulikuwa na matabahu saba (Hesabu 23:1-2,4,14,29; 2Mambo ya nyakati 29:21). Damu ilimiminua mara saba (Lawi 4:6,17; 14:7; 16:14, Hesabu 19:4) na mafuta ya upako yalimiminwa mara saba, (lawi 18:11)



Mapambo ya urembo wa Hekalu kawaida vilikuwa katika haina saba (1 wafalme 7:17 (kutokana na maandiko ya Kimosoreti); Ezekiel 40:22,26; cf. Methali 9:1).



Kinara cha msumaa kilicho na matawi saba, pamoja na sanduku la agano vilikuwa kusudi takatifu la kutazamwa katika Hekalu (kutoka 25:31-37; 1 Wafalme 7:49; Zakaria 4:2,11) Taz pia somo la Sanduku la Agano [196]).

 Image result for holy spirit

Dhana ya viapo imefungamanishwa na saba na watu saba waadhiriwa walipatanishwa kwa kurejesha agano lilovunjika (2 Samuel 21:6,9).



Uchunguzi wahadithi ya Samson uonyesha kwamba alikuwa Mnazirite. Tunaona nywele yake imertibiwa katika shungi saba (Waamuzi 16:13-19).  Kuainishwa huku kunashiria vipengee saba vya Roho ya Mungu ndani ya mtu.



Kwa ajili ya kisasi na adhabu vipengee saba vilipiwa (Mwanzo 4:24; kutoka 7:25; Lawi 26:18; Methali 6:31; Danieli 4:16,23,25).



Saba kutumika kiroho hushinda matokeo ya dhambi na ulimwengu unazamiwa kwa njia za Naaman Yule msiria aliyepona, ambayo ilitenga kukombolewa kwa watu wa mataifa (2 Wafalme 5:10)



Kusudi hili limeelekezwa katika ubatizo kama ondoleo la dhambi na kukubalika kuunganika katika mwili wa Kristo, ambayo ni Hekalu la Mungu.

Kristo kama nahodha wa Jeshi alilenga kushinda dunia kwa matumizi ya msunguko wa saba wa Yeriko (Joshua 6:4,8,14) (Taz. pia masomo haya Kwanguka Kwa Yeriko [142]).

Elisha alifanya maajabu yaliyofuatana, yaliyofunganishwa kweye mfano waKanisa.  Muujiza wake wasaba ulikuwa wa kufufua mtoto.

Mtoto aliyefufuliwa alipiga chafya mara saba na kwa kufanya hivyo aliashiria Roho saba katika kuwafufua wafu na kuwafanya kuwa hai katika uweza wa Roho Matakatifu wa Mungu (Wafalme 35-37).

Muujiza wa nanne wa Elisha ulielekeza kewnye manabii wenyewe.  Kulikuwa na njaa katika nji, ambayo ni moja kati ya njaa kumi na tatu zimetajua katika Biblia (Mwanzo 12:10; 26:1; 41:54; Ruthu 1:1; 2 Samueli 21:1; 1 Wafalme 18:2; 2Walfalme 4:38; 7:4; 25:3; Nehemia 5:3; Yeremia 14:1; Luke 15:14; Matendo 11:28. Kumi natatu ninambari iliyousishwa na uasi na njaa hivyo ilikuwa matokeo ya dhambi na maasi.  Ilikuwa Jumla juhudi za shetani kujaribu kufarakanisha mpango wa mungu na kuruhusiwa katika huo mpangilio.

Moja wa manabii karibu asumishe miili ya manabii waliokuwa waandaa chaku cha mchuzi wa nyama au iliyotokoshwa ambayo Elisha alimwagiza Gehazi kuwandalia.  Nabii mmoja alichukua maboga geni ajabu na akatia katika mchuzi na hapo mwingine akatambua kwamba kulikuwa na kitu chenye sumu katika chungu cha kupikia.  Elisha aliuwa sumu kwakutia chakula ndani ya chungu na kwa jinsi hiyo aliondoa hatari.  Wangejua kuhusu shida  hii wangesuhia isitokee.  Shida ni kuwa moja kati yaya manabii alikuwa chanzo cha sumu katika imani. 

Wazo la wana saba katika maandiko ililenga malaika saba wa Kanisa saba na uduma ya roho saba za Mungu. Matumizi katika kitabu cha Ruthu yanalenga Kristo na Kanisa (Ruth 4:15). Matumizi katika kitabu cha Ayubu yanalenga mwili aliyokuwa nayo na ambao uliondolewa kwa ajili ya dhambi zao na urejesho aliyopokea kama matokeo ya imani. (Ayubu 1:2; 42:13; Tazama pia Matendo 19:14).

Saba zinaushirikiano na nane ambazo utenda kama chombo cha Mungu na ni kama nane. Tunaona upeo huu ukitukia katika kumuusisha Kristo pamoja na kwamba mbona nane ni nambari ya Kristo na saba ni asili ya uduma yake. Wakati Elisha aliomba mara mbili ya roho ya Eliya alifanya miujiza mara mbili zaidi ya hesabu ya miujiza za Eliya aliofanya katika miundo miwili ya nane.

Kumi na mbili ni awamu nyingine ya utimilivu katika uduma.

Ayubu alikuwa na wana saba na kondoo elfu saba.

Mungu alimbariki na akaongezewa kondoo mara mbili na akarejeshewa vijana wake na wasichana watatu.

Ayubu sura 42:

1 Ndipo Ayubu akamjibu Bwana, na kusema. 2 Najua ya kuwa waweza kufanya mambo yote, Na ya kuwa makusudi yako hayawezi kuzuilika. 3 Ni nani huyu afichaye mashauri bila maarifa? Kwa maana, nimesema maneno nisiyoyafahamu, Mambo ya ajabu ya kunishinda mimi, nisiyoyajua. 4 Sikiliza, nakusihi, nami nitanena; Nitakuuliza neno, nawe niambie. 5 Nilikuwa nimesikia habari zako, kwa kusikia kwa masikio; Bali sasa jicho langu linakuona. 6 Kwa sababu hiyo najichukia nafsi yangu, na kutubu Katika mavumbi na majivu. (Biblia Takatifu BT)

Kumcha Mungu ndio mwanzo wa hekima.

7 Basi ikawa, baada ya Bwana kumwambia Ayubu maneno hayo, Bwana akamwambia huyo Elifazi Mtemani, Hasira zangu zinawaka juu yako, na juu ya hao rafiki zako wawili; kwa kuwa ninyi hamkunena yaliyo sawa katika habari zangu, kama alivyonena mtumishi wangu Ayubu. 8 Basi sasa, jitwalieni ng'ombe waume saba, na kondoo waume saba, mkamwendee mtumishi wangu Ayubu, mjisongezee sadaka ya kuteketezwa; na huyo mtumishi wangu Ayubu atawaombea ninyi; kwa kuwa nitamridhia yeye, nisiwatende sawasawa na upumbavu wenu; kwani ninyi hamkunena maneno yaliyonyoka katika habari zangu, kama alivyonena mtumishi wangu Ayubu. 9 Basi Elifazi, Mtemani, na Bildadi, Mshuhi, na Sofari, Mnaamathi, wakaenda, wakafanya kama vile Bwana alivyowaamuru; naye Bwana akamridhia Ayubu. 10 Kisha Bwana akaugeuza uteka wa Ayubu, hapo alipowaombea rafiki zake; Bwana naye akampa Ayubu mara mbili kuliko hayo aliyokuwa nayo kwanza. 11 Ndipo wakamwendea nduguze wote, waume kwa wake, nao wote waliojuana naye hapo zamani, wakala chakula pamoja naye katika nyumba yake; nao wakamlilia na kumtuza moyo katika habari za huo uovu wote Bwana aliouleta juu yake; kila mtu akampa kipande cha fedha, na pete ya dhahabu kila mmoja. 12 Basi hivyo Bwana akaubarikia huo mwisho wa Ayubu zaidi ya mwanzo wake; naye alikuwa na kondoo kumi na nne elfu, na ngamia elfu sita, na jozi za ng'ombe elfu, na punda wake elfu. 13 Tena alikuwa na wana waume saba, na binti watatu. 14 Akamwita huyo wa kwanza jina lake Yemima; na wa pili akamwita jina lake Kesia; na wa tatu akamwita jina lake Keren-hapuhu. 15 Katika nchi hiyo yote hawakuwapo wanawake waliokuwa wazuri kama hao wana wa Ayubu; na baba yao akawapa urithi kati ya ndugu zao wana waume.  16 Kisha baada ya mambo hayo Ayubu akaishi miaka mia na arobaini, naye akawaona wanawe, na wana wa wanawe, hata vizazi vinne. 17 Basi Ayubu akafa, mzee sana mwenye kujawa na siku. (Biblia takatifu BT)

Hapa tunaona kumi na nane kama muundo mara mbili wa saba katika jumla ya kikundi cha mifugo. Jeshi la mbinguni litakuwa maradufu kupitia kwa vitendo vya Roho wa Mungu kupitia usikivu (Taz. masomo Mji Wa Mungu [180]).
Image result for holy spirit

Mpangilio mwingine ni ule wa ngamia elfu sita unaowakilisha miaka elfu sita ya uumbaji najisi chini ya Shetani na ndio wakati ambapo Ayubu alipoteza wana wake wakaidi. Ndume elfu moja na punda za kike elfu moja zinawakilisha awamu ya mwisho ya mfumo wa kipindi cha miaka elfu moja cha Mungu ambayo ni safi. Kuna ndume elfu moja wanaowakilisha jeshi takatifu na elfu moja kuwakilisha jeshi la binadamu wangali wataelimishwa, na pamoja wanawakilisha mfumo wa nane katika sura ya mwisho.

Ayubu pia uorodhesha muundo wa elfu moja kama serikali ya Mungu (Ayubu 3:23).



Unajisi na Utakaso Hadi Upatanisho

Utaratibu wa ibada za unajisi na utakazo pia zilihusisha vipindi vya siku saba, jinsi walivyo fanya katika sherehe za harusi (Warumi 14:12,17; Job 11:19)

Biblia hutumia vipindi vya uduma vya siku saba kama jaribio la usikivu, kati ya mambo mengine (Mwanzo 7:3-4,4,10; 8:10,12; ISamueli 10:8; 11:3; Ezekiel 3:16-17).

Utakazo kwa ibada nzito za unajisi zilidumu siku saba pia (Lawi 15:19,28; Hesabu 19:11,14,16).

Ayubu alionyesha toba halisi na shauku kwa kupatanishwa iliyoashiriwa kwa kufuatanisha kusujudu kwake mara saba mbele ya Esau na kutoa machozi katika bega lake (Mwanzo. 33:1-7).

Kumbukumbu la torati 28:7,25 ina nena kwamba maadui wa Israeli watatoweka katika njia saba.Fungu hili linarejelea mfumo wa njia saba wa Kisumeria ambao badala yake kukawa na mfumo wa njia nne tunaotumia sasa. Sehemu hizi nnezlikuwa mfano wa Cherubim kama viumbe hai wane. Hii ndio asili ya joka za pepo nne za Mbinguni zinavyotatua na Wachina.

Kuhitilafiana kwa mifumo huenda ulitokea hivyo hihli kudhiirisha sababu ya ile dhana ya malaika saba au Roho Saba za Mungu inavyopambanishwa na viumbe hai vine vinavyosunguka kiti cha Enzi cha Mungu.



Sabini

Matumizi ya sabini yameelekezwa katika muundo wa jeshi la Mbinguni na asili ya saba imefunganishwa pale.

Mungu alitumia saba kama nambari ya miaka ya chakula kingi na ya njaa hili kuelekeza dhamiri ya Wamisiri kwa hali yao (Mwanzo 41:1-57; Tazama pia 2 Wafalme 8:1).Yusufu alikuwa chombo cha unabii ambayo ungewakabili. Mungu alimweka Yusufu pale Misiri hili kwamba washuhudiwe nakabila la urithi taifa la Israeli. Taifa la Israeli lingefanyika mwili wa Kristo baada ya muda na katika huo mwili watu wa mataifa wangechopolewa.

Yakobo alienda Misiri akiwa na Jamaa sabini .Pale alikuwa ufunguo wa mwili wa imani na akawa mwanzilishi wa taifa ambalo lilikuwa urithi wa Kristo. Hivyo sabini ukiongesa Kristo na Mungu, walikuwa kielelezo kwa Israeli na Kanisa: wote chini ya Musa na tangu uduma ya Yohana.

Wakati Yakobo alikufa alihifadhiwa kwa kutiwa dawa kwa kipindi cha siku arobaini na hivyo Misiri inakumbukwa kama iliohuzunika juu ya Israeli kwa siku sabini (Mwanzo 50:3)

Idadi hizi zinahusiana na jeshi la Mbiguni. Idadi ya Kafara za wafu za Baal katika hadithi za miungu za kiugariti zilikuwa mfululizo wa minyama sabini. Miungu ya Ugariti kwapamoja imetajua kama wana sabini wa Ashera (Interp. Dict., op. cit., p. 295). Hivyo Baal ya mfumo wa Asteroth pia asili yake ilitokana kwa jeshi la mbiguni sabini na kuitilafiana kujitokeza jinsi mtawanyiko kati ya mungu mama na mfumo wa Baal pamoja na mfumo wa Biblia wa sabini, inavyodhihirishwa katika baraza kuu la Israeli wa zamani (Sanhedrin) Kama sabini na mbili) na katika Kanisa kama sabini na (mbili) au Hebdomekonta(mbili) ya maandiko ya Kigiriki ya Luka 10:1,17.

Musa alikabiliana na miungu ya Misiri mwishoni mwa masikani yao pale Misiri (Taz. Masomo haya Musa na miungu za Misri [105]).

Katika kila mwaka wa saba wa taabu zingekatishwa katikati, kufuatia Mbingu kuingilia kati tokana na toba na huruma za Mungu ama katika  kutimisha mpango wake. Danieli 7:25; 9:27; Luka 4:25; Jas 5:17; Ufunuo 11:12).

Hekima ya Mungu inadumu kwenye nguzo saba. Hiyo hekima hufanya wanyenyekevu kuwafadhahisha wenye uwezo na  kuoyesha umuhimu wa maarifa na kicho au kumhofu Mungu.

Methali 9:1-6 Hekima umeijenga nyumba yake, Amezichonga nguzo zake saba; 2 Amechinja nyama zake, umechanganya divai yake, Ameiandalia meza yake pia. 3Amewatuma wajakazi wake, analia, Mahali pa mjini palipoinuka sana, 4 Kila aliye mjinga na aingie humu. Tena amwambia mtu aliyepungukiwa na akili, 5 Njoo ule mkate wangu, Ukanywe divai niliyoichanganya. 6 Enyi wajinga, acheni ujinga, mkaishi, Mkaende katika njia ya ufahamu. (Biblia Takatifu BT)

Mungu uruhusu kushindwa na kubona katika toba bali wafanyao dhambi maksudi wataangamizwa.

Methali 24:16 Kwa maana mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena; Bali wasio haki hukwazwa na mabaya. (Biblia Takatifu BT)

Kristo alitushauri kusamehe sabini mara sabini katika Mathayo 18:22. Idadi hii pia iliwakilisha kipindi cha majuma sabini ya miaka ambayo Mungu alimtuma Kristo kusihi Yuda wakati wa hawamu kamilivu ya ujenzi na utendaji wa mifumo ya Hekalu katika Danieli 9:25-28 (Tazama masomo haya Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi mpya wa Hekalu [013]).

Kawaida kulikuwa na idadi maalum katika Israeli ambao hawakuinamisha goti kumuabudu Baali na hao waliorodheshwa kama elfu saba au mia moja mara sabini (1 Wafalme 19:18; Warumi 11:4)



Roho wa Mungu Ndani ya Binadamu

Tunajua kwamba roho wa Mungu ndani ya  mwanadamuuonyesha  tabia saba, vile tuliona kutoka Samson hapo juu.Inafikia kiwago chake cha juu katika umbo la ubinadamu ndani ya Masihi. Hata hivyo tabia hizo huelezea uduma zake.



Roho, kamamwangalizi juu ya Dunia, ulitabiriwa na Mungu katika Zakaria.



Zakaria 3:9 Maana, litazame jiwe hili nililoliweka mbele ya Yoshua; katika jiwe moja yako macho saba; tazama, nitachora machoro yake, asema Bwana wa majeshi, nami nitauondoa uovu wa nchi ile katika siku moja. (Biblia Takatifu BT)



Heshima ni kwa Masihi, ambaye ni Yoshwa, anayeitwa Kristo.



Pande saba na taa saba zote zimeelezwa katika Zakaria



Zakaria Sura 4.

1 Na yule malaika aliyesema nami akanijia mara ya pili, akaniamsha, kamamtu aamshwavyo katika usingizi wake. 2 Akaniuliza, Unaona nini? Nikasema, Nimeona, na tazama, kinara cha taa cha dhahabu tupu, nacho kina bakuli juu yake, na taa zake saba juu yake; tena iko mirija saba ya kuleta mafuta, kwa taa zote zilizo juu yake; 3 na mizeituni miwili karibu yake, mmoja upande wa kuume walile bakuli, na mmoja upande wake wa kushoto. 4 Nami nikajibu, nikamwambia yule malaika aliyesema nami, nikasema, Ee Bwana wangu, vitu hivi ni nini? 5 Ndipo malaika aliyesema nami akajibu, akaniambia, Hujui vitu hivi ni nini? Nikasema, La, Bwana wangu. 6 Akajibu akaniambia, akisema, Hili ndilo neno la Bwana kwa Zerubabeli, kusema, Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali ni kwa roho yangu, asema Bwana wa majeshi. 7 Nani wewe, Ee mlima mkubwa? Mbele ya Zerubabeli utakuwa nchi tambarare; naye atalileta lile jiwe la kuwekwa juu kabisa pamoja navigelegele vya, Neema, neema, ilikalie. 8 Tena neno la Bwana likanijia, kusema, 9 Mikono yake Zerubabeli imeiweka misingi ya nyumba hii, namikono yake ndiyo itakayoimaliza; nawe utajua ya kuwa Bwana wa majeshi amenituma kwenu. 10 Maana ni nani aliyeidharau siku ya mambo madogo? Kwa kuwa watafurahi, nao wataiona timazi katika mkono wa Zerubabeli; naam, hizi saba ndizo macho ya Bwana; yapiga mbio huko na huko duniani mwote. 11 Ndipo nikajibu, nikamwambia, Ni nini mizeituni hii miwili iliyo upande wa kuume wa kinara cha taa kile na upande wake wa kushoto? 12 Nami nikajibu mara ya pili, nikamwuliza, Ni nini haya matawi mawili ya mizeituni, ambayo kwanjia ya ile mifereji miwili ya dhahabu hutoa mafuta yao? 13 Akanijibu, akasema, Hujui hivi ni nini? Nikasema, La, Bwana wangu. 14 Ndipo akasema, Hivi ni hao wana wawili wa mafuta, wasimamao karibu na Bwana wa dunia yote. (Biblia Takatifu BT)



Umuhimu wa unabii umeelezwa katika kazi hii:  Ufafanuzi juu ya Zakaria (Nam. 207). Hapa tunakabiliana na uhalisi wa Roho Saba za Mungu zinazodhihirishwa katika jozi saba za macho. Hizi zinaweza kutobainishwa namalaika wa kanisa saba.



Tabia saba za roho zinaonekanakutoka Isaya.



Isaya Sura 11:

1 Basi litatoka chipukizi katika shina la Yese, na tawi litakalotoka katika mizizi yake litazaa matunda. 2 Na roho ya Bwana atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha Bwana; 3 na furaha yake itakuwa katika kumcha Bwana; wala hatahukumu kwa kuyafuata ayaonayo kwa macho yake, wala hataonya kwa kuyafuata ayasikiayo kwa masikio yake; 4 bali kwa haki atawahukumu maskini, naye atawaonya wanyenyekevu wa dunia kwa adili; naye ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake, na kwa pumzi ya midomo yake atawaua wabaya. 5 Na haki itakuwa mshipi wa viuno vyake, na uaminifu mshipi wa kujifungia. (Biblia Takatifu BT)



Mafungu sita ya kwanza ya maandiko ya isaya 11 uonyesha tabia na kwamba zinaashiria Masihi moja kwa moja.



1. Ufahamu namaarifa

2. Ushauri nauwezo

3. Hekima

4. Kicho kwa kumhofu (Yahovah wa Majeshi)       itakuwa manukatob kwake.

5. Wenye haki (hukumu)

6. Usawa

7. Uaminifu



Matokeo ya vidokezo hivi niamani.



6 Mbwa-mwitu atakaa pamoja na mwana-kondoo, na chui atalala pamoja na mwana-mbuzi; ndama na mwana-simba na kinono watakuwa pamoja, na mtoto mdogo atawaongoza. 7 Ng'ombe na dubu watalisha pamoja; watoto wao watalala pamoja; na simba atakula majani kama ng'ombe. 8 Na mtoto anyonyaye atacheza penye tundu la nyoka, na mtoto aliyeachishwa atatia mkono wake katika pango la fira. 9 Hawatadhuru wala hawataharibu katika mlima wangu wote mtakatifu; maana dunia itajawa nakumjua Bwana, kama vile maji yanavyoifunika bahari. (Biblia Takatifu BT)



Hii ni mbinu ya sayuni, mlima wa Mungu, katika Yerusalem. Unabii huu umeenea katika siku za mwisho ambapo mzizi wa Yesse utaongoza watu wake katika uhamisho huu wa pili kutoka mataifa yote.



10 Na itakuwa katika siku hiyo, shina la Yese lisimamalo kuwa ishara kwa kabila za watu, yeye ndiye ambaye mataifa watamtafuta; na mahali pake pa kupumzikia patakuwa na utukufu. 11 Na itakuwa katika siku hiyo, Bwana atapeleka mkono wake mara ya pili, ili ajipatie watu wake watakaosalia, kutoka Ashuru, na kutoka Misri, na kutoka Pathrosi, na kutoka Kushi, na kutoka Elamu, na kutoka Shinari, na kutoka Hamathi, na kutoka visiwa vya bahari. 12 Naye atawatwekea mataifa bendera, atawakutanisha watu wa Israeli waliotupwa, atawakusanya watu wa Yuda waliotawanyika, kutoka ncha nne za dunia. (Biblia Takatifu BT)



Wakati huo roho waMungu utadumu juu ya Israel na Yuda na watakuwa pamoja.



13 Na wivu waEfraimu utaondoka, na wale wanaomwudhi Yuda watakatiliwa mbali; Efraimu hatamhusudu Yuda, wala Yuda hatamwudhi Efraimu. (Biblia Takatifu BT)



Israel itakuwa naamani na itazunguka nchi ya Waifilipi ikiunganisha Gaza. Watamilki Yorodani ambayo itakuwa sehemu ya Israel kuu katika amani. Geografia   ya Bahari nyekundu itabatilishwa, inaminika kwa matukio ya mtetemeko wa ardhi unaonekana kila pahali na katika unabii wa mizeituni. Masihi atakabiliana naAram kwa upande wa Frati na shatter kwa upande wa kuingia kwenye mifereji saba na watu watatembea juu ya nchi kavu.



14 Nao watashuka, watalirukia bega la Wafilisti upande wamagharibi; nao pamoja watawateka wana wa mashariki; watanyosha mkono juu ya Edomu na Moabu; na wana wa Amoni watawatii. 15 Na Bwana atauangamiza kabisa ulimi wa bahari ya Misri; na kwa upepo wake uteketezao atatikisa mkono wake juu ya Mto, naye ataupiga, uwe vijito saba, na kuwavusha watu wenye viatu vikavu. 16 Itakuwako njia kuu kwamabaki ya watu wake watakaobaki, watokao Ashuru, kama vile ilivyokuwako kwa Israeli, katika siku ile waliyotoka katika nchi ya Misri. (Biblia Takatifu BT)



Nchi yote tangia mahali wanataja kuwa Iraq hadi Misiri itaunganishwa na hili ni katika amani.



Mifereji saba uelekeza kuzuiliwa kwa Frati, ambapo ndipo kiti cha Shetani  kilikuwa wakati wa utawala wa Babuloni, hadi vijito saba iliowezeza watu wake kuishi kwa amani na wakapata njia ya kufikia kwa inchi takatifu na Hekalu la Mungu.



Sehemu Saba za maombi kama Roho wa Mungu

Tabia saba za Roho wa Mungu  pia zimewakilishwa na ombi la Suleiman kama kipeo  cha ujenzi wa Hekalu ambaye ni  mwana wa Daudi (1Wafalme 8:29–53) na ile ya Kristo hikiwa hitimisho kwa mjenzi wa Hekalu  Halisi la Mungu  (Matayo 6:9-13) (Tazama pia Utawala wa Wafalme sehemu ya III: Suleiman na ufunguo wa Daudi (Nam. 282C)).



Solomon

1 Wafalme 8:29-53 Macho yako yafumbuke na kuielekea nyumba hii usiku na mchana, mahali hapa ulipopataja, ukasema, Hapa ndipo litakapokuwapo jina langu; ili uyasikie maombi ya mtumwa wako aombapo akikabili mahali hapa. 30 Uisikie dua ya mtumwa wako, na ya watu wako Israeli, watakapoomba wakikabili mahali hapa; naam, sikia huko mbinguni, makao yako; nawe usikiapo, samehe. 31 Ikiwa mtu amemkosa mwenzake, na kupewa sharti ya kiapo aapishwe, naye akija na kuapa hapa mbele ya madhabahu yako, katika nyumba hii; 32 basi, usikie huko mbinguni, ukatende, ukawahukumu watumwa wako; ukimpatiliza mtu mbaya, kwa kuleta njia yake juu ya kichwa chake; na kumpa mwenye haki haki yake, ukimjalia kwa kadiri ya haki yake. 33 Ikiwa watu wako Israeli wamepigwa mbele ya adui zao, kwa sababu wamekukosa wewe; kama wakirejea tena kwako, na kulikiri jina lako wakikuomba na kukusihi katika nyumba hii; 34 basi, usikie huko mbinguni, ukawaachilie watu wako Israeli dhambi yao, ukawarejeze tena katika nchi uliyowapa baba zao. 35 Ikiwa mbingu zimefungwa, hata hakuna mvua, kwa sababu wamekukosa wewe; kama wakiomba wakikabili mahali hapa, na kulikiri jina lako, na kuiacha dhambi yao, wakati ule utakapowatesa; 36 basi, usikie huko mbinguni, ukaisamehe dhambi ya watumwa wako, na ya watu wako Israeli; unapowafundisha njia iliyo njema, iwapasayo kuiendea; ukanyeshe mvua juu ya nchi yako, uliyowapa watu wako iwe urithi wao. 37 Ikiwa nchi imeingia njaa, au tauni, au ukosefu wa mvua, au ukungu, au nzige, au panzi; ikiwa adui wamewahusuru katika nchi ya miji yao; au ukiwapo msiba wo wote, au uele wo wote; 38 maombi yo yote au dua yo yote ikifanywa na mtu awaye yote, au na watu wako Israeli wote pamoja, watakaojua kila mtu maradhi ya moyo wake, na kuikunjua mikono yake kuielekea nyumba hii; 39 basi, usikie huko mbinguni, makao yako, ukasamehe, ukatende, ukampe kila mtu kwa kadiri ya njia zake; wewe ujuaye moyo wake; (maana wewe peke yako ndiwe uijuaye mioyo ya wanadamu wote); 40 ili wakuche wewe siku zote watakazoishi katika nchi uliyowapa baba zetu. 41 Hata na mgeni naye, asiyekuwa mmoja wa watu wako Israeli, atakapokuja kutoka nchi iliyo mbali sana kwa ajili ya jina lako; 42 (maana watasikia habari za jina lako kuu, na za mkono wako ulio hodari, na za mkono wako ulionyoshwa); atakapokuja na kuomba kuielekea nyumba hii; 43 basi, usikie huko mbinguni, makao yako, ukatende kwa kadiri ya yote atakayokuomba mgeni huyo; ili watu wote wa dunia wapate kulijua jina lako, na kukucha wewe kama watu wako Israeli, nao wajue ya kuwa nyumba hii, niliyoijenga, imeitwa kwa jina lako. 44 Ikiwa watu wako watoka kwenda kupigana na adui zao, kwa njia yo yote utakayowapeleka, wakikuomba, Bwana, kuuelekea mji huu uliouchagua, na nyumba hii niliyoijenga kwa jina lako; 45 basi, uyasikie huko mbinguni maombi yao na dua yao, ukaitetee haki yao. 46 Ikiwa wamekutenda dhambi, (maana hakuna mtu asiyetenda dhambi), hata ukawaghadhibikia, ukawatia katika mikono ya adui zao, wawachukue mateka mpaka nchi ya adui zao, iliyo mbali au iliyo karibu; 47 basi, wakijirudia nafsi zao katika nchi ile watakayochukuliwa mateka, wakitubu, na kukusihi katika nchi ya hao waliowachukua mateka, wakisema, Tumekosa, tumefanya ukaidi, tumetenda maovu; 48 watakaporejea kwako kwa mioyo yao yote, na kwa nia zao zote, katika nchi ya adui zao, waliowachukua mateka, wakikuomba, kwa kuikabili nchi yao, uliyowapa baba zao, na mji huu uliouchagua, na nyumba hii niliyoijenga kwa jina lako; 49 basi, uyasikie maombi yao na dua yao, huko mbinguni, makao yako, ukaitetee haki yao; 50 ukawasamehe watu wako waliokutenda dhambi, na makosa yao yote waliyokukosa; ukawape kuonewa huruma mbele yao waliowachukua mateka, ili wapate kuwahurumia. 51 Kwa kuwa ni watu wako, na urithi wako, uliowatoa katika Misri, toka katikati ya tanuu ya chuma. 52 Macho yako na yafumbuke, na kuielekea dua ya mtumwa wako, na dua za watu wako Israeli, ukawasikilize kila wakati watakapokulilia. 53 Kwa maana uliwatenga na watu wote wa dunia, wawe urithi wako, kama ulivyonena kwa mdomo wa Musa, mtumishi wako, hapo ulipowatoa baba zetu katika Misri, Ee Bwana MUNGU. (Biblia Takatifu BT)



Kuomba kumewekwa sehemu nne ikiwa na vikato saba inavyofuata.



Katika Nafsi

31. Mada hatia kwa kumukosea jirani yako kutokana maelekezo katika vitabu vitano vya sheria  

32. “Zkia Ninyi” kusihi kwa hukumu takatifu amabyo uwahadhibu wenye dhambi na kuwapa haki wasio na hatia.



Maneno “kufanywa kulakiapo” yameondolewa kutoka tafsiri za Kiarama, Kisyria, Maandiko ya Kiebrania ya karne ya tatu kabla ya kuzaliwa kwa Yesu na kwa lugha ya kiasili



Katika Taifa

33. Mada maombi (kulingana na lawi 26:17; Kumbu. 28:25) watu wanapotegwa na dhambi na kwaguka wanamugeukia Mungu.

34. “Enyi Sikia” walete tena (Kumbukumbu 30:1-8; Nehemiah 1:8,9) wakomboe.

35. Mada wakati mbingu zimefungwa na hakuna mfua (Lawi 26:19; Kumbukumbu 11:17, cf. 17:1)

36. “Enyi Sikia” kwamba ninyi wafundishe – sababu ninyi mtafundisha (c.f Bullinger). Wafundishe wafahamu dhambi zao na haki.

37-38. kukiwa na maradhi, mlibuko mkubwa na nzige au mdudu (mafa na  maangamizi ) au ikiwa wamezingirwa kwa vita (Lawi 26:26)

39-40. “Enyi Sikia”  washughulikie watu (adamu) na wageni na wakaaji wa nchi geni (c.f nambari 15:14; Kumbukumbu 10:19) sikia maombi ya mtu yeyote au kundi la watu na upate kufahamu shida zilizo moyoni na umtendee kulingana na jinsi alivyo ili waweze kuwa na kicho na kumhofu  Mungu.



Katika nafsi

41-42. Mada: wageni watasikia jina lako tukufu na waingie wakasali katika Hekalu la Mungu.

(cf. 10:1,6,7)

43. “Enyi Sikia” zikiliza katika makao yenu pale Mbinguni na mfanye mgeni atakavyo waomba hili kwa hilo jina lenu litaheshimiwa au kuhofiwa na mataifa yote jinsi ilivyo katika Israel.



Katika Taifa

44. Mada: Ulinzi dhidi ya adui katika vita kwa ajili ya injili ya maombi na kutazama mbele pale Hekaluni mwa Mungu.

45. “Enyi Sikia” fanya uamuzi wa kesi zao kwa kuwasikiliza huku mkidumisha kusudi lao.

46-48. Mada: ikiwa watawakosea kwa kuwa hakuna yeyote amewakosea na wakapelekwa mateka na wakatubu pale matekani na kukiri dhambi zao na kurudi na moyo wao wote na kuomba kuekea Hekalu (c.f Methali 20:9, Muhubiri 7:20, Yoshua 3:2, 1Yohana 1:8,10).

49-53 “Enyi Sikia” wasamehe dhambi zao pamoja na uasi wao. Wahurumie mbele ya watesi. Myasikie malalamiko ya watu wenu Israeli jinsi mlivyo walaki kutoka duniani wawe watu wateule.



Bullinger pia anagusia muundo huu.



Mafundisho ya Kristo na Maombi

Kinachotajwa kamaombi la Mungu katika Matayo 6:9-13 maana yake ni ratiba ya maelekezo ya jinsi ipaswavyo kupangilia ombi. Ni muundo wa cheti na haichanuiwa kutumika peke yake kama ombi la kukariri jinsi imani nyingi zinalitumia.



Inatukia katika mpangilio wa Tangia 6:1 hadi 7:11 ambayo maana yake ushambulia mazoea ya wazee.

6:2- 4   kuhusu matoleo

6:5- 15 kuhusu ombi

6:10- 10 kuhusu kufunga

6:19- 24 kuhusu utajiri

6:25- 7:11 kuhusu kutunza ulimwengu



Matayo 6:9-13 Basi ninyi salini hivi; Baba yetu  uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje, 10 Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni. 11 Utupe leoriziki yetu. 12 Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu. 13 Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina. (Biblia Takatifu BT)



Asili ya maelekezo haya ni:



1.      Kuomba Mungu moja kwa moja kwa  siri.

2.      Kutoa maombi rahisi moja kwa moja si kwa kukariri au maombi ya kila siku na katika taarifa.

3.      Mungu ufahamu utakajo kabla ujaomba.



Vibengee vya maombi

1.      Muhimidi Baba aliye Mbinguni na   hivyo kumhofu Mungu na kutakaza jina lake (Kutoka 4:22; Kumbu 32:6-8). Wenye ibada za sanamu walisujudu sanamu zao wakisema:  “we ndiye baba yangu” na Israeli wakafuata hii mienendo na kufanya hivyo pia. (Isaya 63:16; 64:8).



2.      Ufalme wako uje Bwana alisema haya wakati wa kugeushwa kwake na ndio ilikuwa kusudi la huduma yake; lakini Yuda waliukataa. Inavizia neno la Mungu sasa.



3.      Mapenzi yako yatimishwe duniani jinsi ilivyo Mbinguni neon. Mbinguni hapa lipo katika hali ya umoja sababu ya kubainisha kati ya mbingu nadunia, lakini katika fungu la 9 iko katka hali ya wingi ili isionyeshe kwamba baba alikuwa Mbinguni na wala si duniani. Katika maneno ya mafungu ya kikgiriki kuna maana iliyokuwa kinyume ilivyo Mbinguni naduniani iwe hivyo.



4.      Utupe leo sote chakula chetu cha kila siku na mahitaji yetu ya kiroho Neno hili kila siku ni la kigiriki ambalo  epiousios. Ni muunganiko wa maneno  amabayo yanaonekana mara mbili  tu katika angano jipya (pia Luka 11:3) na yalibuniwa na Kristo kama muungano kutoka epi juu ya ousius inamaanisha kuja.Kwenye fungu moja la kurasa  za Bullinger anashikilia kwamba umaanisha kuja au kushuka kutoka juu ilivyofanyika pale jangwani wakati manna ilianguka na imetofautiana katika Yohana 6:32,33.  Kwa hivyo huu ni mkate halisi kutoka mbinguni, hivyo basi kujumuisha neno la Mungu. Mtu hataishi kwa mkate tu bali kwa kila andiko litokalo kwa kinywa cha Mungu.



5.      Tusamehe makosa yetu na dhambi zetu tunayofanya kwa kuwa hakuna mtu hawezi fanya dhambi. Nasi vivyo hivyo tunawasamehe wanaotukosea hili nasi pia tupate msamaha. Dhambi ni deni hivi kwamba huitaji kulipiwa. Kristo alilipa madeni ya wenye dhambi wote na tunawezeshwa kwenda mbele za Mungu hili kupokea ondoleo la dhambi ambapo hukumu ya kuwiwa  deni  iligongelewa msalabani (chierographon) kwa hisa au stauros.  Muundo wa rehema lasima uwepo kwa kuwa hii ni sehemu ya matoleo ya Masihi katika kutekeleza vipengele saba vya Roho tendaji katika mwanadamu.



6.      Usitutie (kutuachilia) katika (majaribu cf. Jas 1:12-13) bali utuokoe na yule mwovu.



7.      Wimbo wa kumsifu Mungu na kuanzisha utawala wake na utukufu milele.



Kipengee hiki cha saba ni muhimu katika muundo  kamili wa maombi kwenye orodha 500 ya kanuni ambayo imejumuisha ombi  na orodha nane tu ambazo zimewacha nche ya  wimbo  wa kumsifu Mungu (cf.  fn. kwa Bullinger, mwandamizi wa Bibilia). Si vyema  kuihebuka na hivyo kudunisha maaana ya maombi kwa utukufu mkuu wa Mungu. Bora zadi upatikana pia katika tafsiri za Syria, Ethopia, Uarmeni, Ugothi, Uslovani na Georgia.



Vipengele vyote vinao upishi kwa mapenzi ya Mungu na pia shida kwenye maombi kwa utendaji halisi wa Roho wa Mungu.



Esta

Esta pia uonyesha hadithi ya Kanisa katika uhusiano wake na Mungu, Malkia Vashti (kipepeo kilicho bora) alidharau mwaliko wa mfalme kwa kuwa mkali kwa wahasi saba waliotumwa kwake (Esta 1:10-12) anawakilisha mataifa onekanevu ya Israeli.



Wahasi sabawanawakilisha malaika saba na makanisa saba.



Esta anawakilisha Kanisa ambalo limeifhadhiwa kwa ajili ya Yesu Kristo ambaye anawakilishwa na Modekai Myahudi. Esta yuna wajakasi saba wateule (Esta 2:9). Wanawakilisha mgawo wa makanisa saba ya Mungu Yanayonekana katika ufunuo.



Esteri hana baba wala mama sababu yeye ni kanisa la utaratibu wa melkisedeki ambayo haina baba wala mama, na ambayo Kristo ni kuhani mkuu jinsi Modekai ni kichwa cha nyumba (Taz. Zaburi 11:4; Waebrania 5:6,10; 6:20; 7:1-21 na masomo haya Melkizedeki (Nam. 128)).



Binadamu Mwagagi navijana wake uwakilisha Shetani na jeshi liloanguka na watumizi waliokuwa miongoni mwao.



Umuhimu huu umedokezwa katika masomo haya Ufafanusi kuhusu Esta (Nam. 63).



Hekalu saba za Bibilia

Katika 1Samueli 1:9 tunaona kicho kwa Hekalu au jumba la mfalme (heykal) ya Bwana, ambapo Eli aliweka kiti chake mlangoni.



Hii ilikuwa heshima ya kwanza kati ya heshima saba kwa Hema kama Hekalu  la Bwana katika Bibilia. Kunayo pia heshima saba katika agano Jipya kwa waumini kama Hema ya Bwana.



1.      Hema imerejelewa katika 1 Samueli  1:9.

2.      Hekalu lilojengwa na Suleimani  limerejelewakatika 1 Wafalme 6:5,17.

3.      Hekalu lililojengwa chini ya Zerubabeli limerejelewa katika Ezra 4:1,2.

4.      Hekalu la wakati wa Herode limerejelewa katika Yohana 2:20. Mpangilio wa Hekalu tatu onekanevu umeelezwa katika masomo haya Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi mpya wa Hekalu [013].

5.      Hekalu la baadaye la kambu limerejelewa katika 2 Wathesaloniki 2:4, ambayo mtu wa dhambi amedhihirishwa kwamba anakaa katika Hekalu ambayo ni Hekalu la Mungu, akijitangaza mwenyewe kwamba yeye ni Mungu.

6.      Hekalu la miaka elfu moja limerejelewa katika Ezekieli  41:1 na,

7.      Hekalu la mwisho la Mbinguni lipo katika ufunuo 21:3,22.



Marejeleo haya saba kwa wawaumini kama Hekalu la Mungu katika Agano Jipya ndio  haya:

1 Wakorintho 3: 9-17 na 6:19; 2 Wakorintho 6:16; Waefeso 2:20,21; Waebrania 3:6; 1 Petero 2:5 na 4:17.



Mlolongo huu tena unadokeza kanuni ya kwamba Roho Saba za Mungu zinadhihirika katika wateule kama Hekalu, na mlolongo ule wa saba utia nguvu unabii uhalisi, kiroho  pia kimawazo.



Roho Saba na Malaika wa Kanisa Saba

Tutaona kuwa muundo waufunuo sura ya kwanza umekatwa katika hawamu mbali mbali kwenye asili ya muundo saba na nane ambao unawakilisha Roho Saba za Mungu chini ya Kristo na vile na nne katika kiti cha Enzi cha Mungu.



Ufunuo sura 1:

1 Ufunuo wa Yesu Kristo, aliopewa na Mungu        awaonyeshe watumwa wake mambo ambayo kwamba hayana budi kuwako upesi; naye akatuma kwa mkono wa malaika akamwonyesha mtumwa wake Yohana; 2 aliyelishuhudia Neno la Mungu, na ushuhuda wa Yesu Kristo, yaani, mambo yote aliyoyaona. 3 Heri asomaye na wao wayasikiao maneno ya unabii huu, na kuyashika yaliyoandikwa humo; kwa maana wakati u karibu. 4 Yohana, kwa yale makanisa saba yaliyoko Asia; Neema na iwe kwenu na amani, zitokazo kwake yeye aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja; na zitokazo kwa roho saba walioko mbele ya kiti chake cha enzi; 5 tena zitokazo kwa Yesu Kristo, shahidi aliye mwaminifu, mzaliwa wa kwanza wa waliokufa, na mkuu wa wafalme wa dunia. Yeye atupendaye na kutuosha dhambi zetu katika damu yake, 6 na kutufanya kuwa ufalme, na makuhani kwa Mungu, naye ni Baba yake; utukufu na ukuu una Yeye hata milele na milele. Amina.(Biblia Takatifu BT)



Sehemu ya kwanza hipo katika muundo wa fungu la 6, ambayo ushungulika na kuteuliwa kwa wateule kama ufalme wa makuhani wa Mungu na Babake Kristo. Hivyo sita ni nambari ya mwanadamu na amina. Yohana ananena kwa makanisa saba jinsi alivyoelekezwa naye Kristo pia Roho Saba kutoka mbele ya kiti cha Enzi cha Mungu, Sehemu ya kwanza imeisha  katika mlolongo wa sita sababu hipo katika mwisho  wa miaka elfu sita ya utawala wa Shetani  na mwisho umewadia ukibashiriwa na amina. Tena tumeambiwa, “tazama yuaja upesi” katika fungu la saba. Mtawanyiko huu si vivi hivi tu bali ni nyongesha kwa bahati mbaya -  yanafuata muundo wa maandishi.



7 Tazama, yuaja namawingu; na kila jicho litamwona, na hao waliomchoma; na kabila zote za dunia wataomboleza kwa ajili yake. Naam. Amina.8 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, asema Bwana Mungu, aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi. (Biblia Takatifu BT)



Fungu la sabalimetamatika na amina.



Fungu la nane tanagazo la utawala mkuu wa Mungu kama Alfa na Omega. Mada hii baadaye ilitiwa katika utendaji wa Masihi kupitia ufunuo (Taz. Masomo haya Asili ya uumbaji  wa Mungu kama Alfa na  Omega (Nam. 229)):

Tena tunaingia katika muundo wa fungu linalofuata la nane, ambalo linaeleza uashirio .



9 Mimi Yohana, ndugu yenu na mwenye kushiriki pamoja nanyi katika mateso na ufalme na subira ya Yesu Kristo, nalikuwa katika kisiwa kiitwacho Patmo, kwa ajili ya Neno la Mungu, na ushuhuda wa Yesu. (Biblia Takatifu BT)



Yohana akiwa nyikani alisema, na hapo akaanza kunena juu ya siku ya Bwana. Hii siyo siku ya juma bali ni ya mwisho wa mpangilio ulio chini ya Shetani (Tazama siku ya Bwana na Siku za Mwisho (No. 192)).



10 Nalikuwa katika Roho, siku ya Bwana; nikasikia sauti kuu nyuma yangu, kama sauti ya baragumu, 11 ikisema, Haya uyaonayo uyaandike katika chuo, ukayapeleke kwa hayo makanisa saba: Efeso, na Smirna, na Pergamo, na Thiatira, na Sardi, na Filadelfia, na Laodikia. 12 Nikageuka niione ile sauti iliyosema nami. Na nilipogeuka, niliona vinara vya taa sabavya dhahabu; 13 na katikati ya vile vinara nikaona mtu mfano wa Mwanadamu, amevaa vazi lililofika miguuni, na kufungwa mshipi wa dhahabu matitini. 14 Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe, kama theluji; na macho yake kama mwali wa moto; 15 na miguu yake kama shaba iliyosuguliwa sana, kana kwamba imesafishwa katika tanuru; na sauti yake kama sauti ya maji mengi.16 Naye alikuwa na nyota saba katika mkono wake wa kuume; na upanga mkali, wenye makali kuwili, ukitoka katika kinywa chake; na uso wake kama jua liking'aa kwa nguvu zake. (Biblia takatifu BT)



Yohana ametaja makanisa saba na kutambua muundo wa nane ,ambayo ni minara ya dhahabu ya taa saba na nane ni mwana wa Mungu ambaye amesimama katikati yao na ndiye mwelekezi. Pia yupo na nyota saba mkononi.



17 Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kamamtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho, 18 na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu. 19 Basi, uyaandike mambo hayo uliyoyaona, nayo yaliyopo, na yale yatakayokuwa baada ya hayo. 20 Siri ya zile nyota sabaulizoziona katika mkono wangu wa kuume, na ya vile vinara saba vya dhahabu. Zile nyota saba ni malaika wa yale makanisa saba; na vile vinara saba ni makanisa saba. (Biblia Takatifu BT)



Hapa katika muundo wa mafungu manne Kristo anaelezea nyota saba kama malaika wa makanisa saba na kuonyosha kuwa minara ya dhahabu ya taa saba ni makanisa saba.



Hivyo kila kanisa nimnara ambao una malaika anayewajibika. Neno ni aster (SGD 792) na limetumika sawa jinsi limetumika katika nyota za jeshi popote kwenye maadiko. Neno anakuja kwenye asili ya stronummi (hivyo astronomy), ambayo kawaida maana yake ni kutawanya au kumwanga. Neno hili linatumika kwa ajili ya jeshi sababu ni kazi yao kueneza hekima ya Mungu wakiwa minara, ambayo ni kanisa itafanya hivyo.



Roho mtakatifu nimfariji wa kanisa na ndiye hutibithi Roho saba za Mungu ndani yake. Utoka kwa Mungu kupitia kwa Kristo kuelekea kwa wateule.



Ni maana ya mto uliotawanyika katika mifereji saba hili binadamu waweze kufikia ule mto na kuutumia kwa ajili ya utukufu wa Mungu na kufanyika wana wa Mungu.



Sura mbili zinazofuata zinashughulika na makanisa saba na yanaelezwa kwa kina katika maandiko haya Nguzo za Filadelfia [283].



Ni bora kufahamu katika hili fungu kuwa ujumbe wa malaika kwa Kanisa saba ni uwajibikaji wa malaika hili kuakikisha ujumbe umefahamika.



Hizi si tu Kanisa sabazilizo kando kando. Bali pia uwakilishi halisi wa Roho saba za Mungu zikiwemo katika kila Kanisa na kwamba kila Kanisa lina vipengee vyote saba kati yao.



Muundo huu huko pia katika mpangilio wa saba kewnye ujumbe kwa Kanisa la Efeso.



Ufunuo, Sura 2:



1 Kwa malaika wa kanisa lililoko Efeso andika;  Haya ndiyo anenayo yeye azishikaye hizo nyota     saba katika mkono wake wa kuume, yeye aendaye katikati ya vile vinara saba vya dhahabu. 2 Nayajua matendo yako, na taabu yako, na subira yako, na ya kuwa huwezi kuchukuliana na watu wabaya, tena umewajaribu wale wajiitao mitume, nao sio, ukawaona kuwa waongo; 3 tena ulikuwa na subira na kuvumilia kwa ajili ya jina langu, wala hukuchoka. 4 Lakini nina neno juu yako, ya kwamba umeuacha upendo wako wa kwanza. 5 Basi, kumbuka ni wapi ulikoanguka; ukatubu, ukayafanye matendo ya kwanza. Lakini, usipofanya hivyo, naja kwako, nami nitakiondoa kinara chako katika mahali pake, usipotubu. 6 Lakini unalo neno hili, kwamba wayachukia matendo ya Wanikolai, ambayo namimi nayachukia. 7 Yeye aliye nasikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye, nitampa kula matunda ya mti wa uzima, ulio katika bustani ya Mungu. (Biblia Takatifu BT)



Katika mpangilio unaofuata wa saba tunaendelea katika ujumbe kwa Kanisa la Simurina.



8 Na kwa malaika wa kanisa lililoko Smirna andika; Haya ndiyo aneneyo yeye aliye wa kwanza na wa mwisho, aliyekuwa amekufa, kisha akawa hai. 9 Naijua dhiki yako na umaskini wako, (lakini u tajiri) najua na matukano ya hao wasemao ya kuwa ni Wayahudi, nao sio, bali ni sinagogi la Shetani. 10 Usiogope mambo yatakayokupata; tazama, huyo Ibilisi atawatupa baadhi yenu gerezani ili mjaribiwe, nanyi mtakuwa na dhiki siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima.
11 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye hatapatikana na madhara ya mauti ya pili. 12 Na kwa malaika wa kanisa lililoko Pergamo andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye na huo upanga mkali, wenye makali kuwili. 13 Napajua ukaapo, ndipo penye kiti cha enzi cha Shetani; nawe walishika sana jina langu, wala hukuikana imani yangu, hata katika siku za Antipa shahidi wangu, mwaminifu wangu, aliyeuawa kati yenu, hapo akaapo Shetani. 14 Lakini ninayo maneno machache juu yako, kwa kuwa unao huko watu washikao mafundisho ya Balaamu, yeye aliyemfundisha Balaki atie ukwazo mbele ya Waisraeli, kwamba wavile vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na kuzini. 15 Vivyo hivyo wewe nawe unao watu wayashikao mafundisho ya Wanikolai vile vile. 16 Basi tubu; na usipotubu, naja kwako upesi, nami nitafanya vita juu yao kwa huo upanga wa kinywa changu. (Biblia Takatifu BT)



Fungu la mwisho nimwaliko wa kutubu. Fungu lifuatalo halianzishi mpangilio unaofuata bali utia nguvu ujumbe wa Mungu kwa mpangilio wote wa makanisa na si tu kwa moja.



17 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa, nami nitampa jiwe jeupe, na juu ya jiwe hilo limeandikwa jina jipya asilolijua mtu ila yeye anayelipokea. (Biblia takatifu BT)



Mpangilio unaofuata umeazia msitari wa 18:

18 Na kwa malaika wa kanisa lililoko Thiatira andika; Haya ndiyo anenayo Mwana wa Mungu, yeye aliye na macho yake kama mwali wa moto, na miguu yake mfano wa shaba iliyosuguliwa sana. 19 Nayajua matendo yako na upendo na imani na huduma na subira yako; tena kwamba matendo yako ya mwisho yamezidi yale ya kwanza. 20 Lakini nina neno juu yako, ya kwamba wamridhia yule mwanamke Yezebeli, yeye ajiitaye nabii na kuwafundisha watumishi wangu na kuwapoteza, ili wazini na kula vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu. 21 Nami nimempa muda ili atubu, wala hataki kuutubia uzinzi wake. 22 Tazama, nitamtupa juu ya kitanda, na hao wazinio pamoja naye, wapate dhiki kubwa wasipotubia matendo yake; 23 nami nitawaua watoto wake kwa mauti. Na makanisa yote watajua ya kuwa mimi ndiye achunguzaye viuno na mioyo. Nami nitampa kila mmoja wenu kwa kadiri ya matendo yake. 24 Lakini nawaambia ninyi wengine mlioko Thiatira, wo wote wasio na mafundisho hayo, wasiozijua fumbo za Shetani, kama vile wasemavyo, Sitaweka juu yenu mzigo mwingine. 25 Ila mlicho nacho kishikeni sana, hata nitakapokuja. 26 Na yeye ashindaye, na kuyatunza matendo yangu hata mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa, 27 naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, kama vyombo vya mfinyanzi vipondwavyo, kama mimi nami nilivyopokea kwa Baba yangu. 28 Nami nitampa ile nyota ya asubuhi. 29 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. (Biblia Takatifu BT)



Mpangilio waThiatira umo kwenye mpangilio kamilifu wa kumi na mbili .Mistari kumi na moja ya kwanza imeelekezwa kwa Thiatira lakini msitari wa kumi na mbili unaedelea kuzigatia kwamba Roho ananena kwa makanisa ya Mungu.



Ufunuo, Sura 3:

1 Na kwa malaika wa kanisa lililoko Sardi andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye na hizo Roho saba za Mungu, na zile nyota saba. Nayajua matendo yako, ya kuwa una jina la kuwa hai, nawe umekufa.2 Uwe mwenye kukesha, ukayaimarishe mambo yaliyosalia, yanayotaka kufa. Maana sikuona matendo yako kuwa yametimilika mbele za Mungu wangu. 3 Basi kumbuka jinsi ulivyopokea, na jinsi ulivyosikia; yashike hayo na kutubu. Walakini usipokesha, nitakuja kama mwivi, wala hutaijua saa nitakayokuja kwako. 4 Lakini unayo majina machache katika Sardi, watu wasioyatia mavazi yao uchafu. Nao watakwenda pamoja nami hali wamevaa mavazi meupe, kwakuwa wamestahili. 5 Yeye ashindaye atavikwa hivyo mavazi meupe, wala sitalifuta kamwe jina lake katika kitabu cha uzima, nami nitalikiri jina lake mbele za Baba yangu, na mbele ya malaika zake. 6 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. (Biblia Takatifu BT)



Fahamu kwamba Saridi imo katika mlolongo wa sita, ambao ni idadi ya wanadamu, na umekufa. Na hivyo Roho wa Mungu hajakamilisha jukumu lake katika mafundisho haya.



7 Na kwa malaika wa kanisa lililoko Filadelfia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye mtakatifu, aliye wa kweli, aliye na ufunguo wa Daudi, yeye mwenye kufungua wala hapana afungaye, naye afunga wala hapana afunguaye. 8 Nayajua matendo yako. Tazama, nimekupa mlango uliofunguliwa mbele yako, ambao hapana awezaye kuufunga, kwakuwa unazo nguvu kidogo, nawe umelitunza neno langu, wala hukulikana jina langu. 9 Tazama, nakupa walio wa sinagogi la Shetani, wasemao kwamba ni Wayahudi, nao sio, bali wasema uongo. Tazama, nitawafanya waje kusujudu mbele ya miguu yako, na kujua ya kuwa nimekupenda. 10 Kwa kuwa umelishika neno la subira yangu, mimi nami nitakulinda, utoke katika saa ya kuharibiwa iliyo tayari kuujilia ulimwengu wote, kuwajaribu wakaao juu ya nchi. 11 Naja upesi. Shika sanaulicho nacho, asije mtu akaitwaa taji yako. 12 Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe, lile jipya. (Biblia Takatifu BT)



Filadefia pia imo kwenye mlolongo wa sita ambao umechipuka toka Saridis na umekamilisha mlolongo wa kumi na mbili. Na tena inayo kipengee cha saba ambacho kimeongezewa kwa ujumbe wake ambao pia unauzingatia kwamba Roho ananena kwa makanisa yote ambayo yamethihirishwa na makabila  kumi na mbili na wa mitume kumi na mbili ambao wanaongoza hayo makabila kama miundo msingi ya Hekalu ya Mungu.



13 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. (Biblia Takatifu BT)



Mpangilio wa saba umeaza na ujumbe kwa Laodekia.

14 Na kwa malaika wa kanisa lililoko Laodikia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye Amina, Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli, mwanzo wa kuumba kwa Mungu. 15 Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kamaungekuwa baridi au moto. 16 Basi, kwasababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu. 17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi. 18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona. 19 Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu. (Biblia Takatifu BT)



Mara nyingi tena mpangilio huu umo katika sita ukitamatika na mwaliko wa toba. Wa saba ni mwaliko wa kuitikia ahadi ya Kristo kuingia na kula naye. Ndio kusema, kumukomboa kila mwaka kwa toba kwa kula meza ya Bwana.



20 Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami. (Biblia Takatifu BT)



Fungu la nane katika mlolongo hapo hutoa ujumbe wa ahadi ya ushindi kutiliwa shaka.

  
21 Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi. (Biblia Takatifu BT)



Mstari wa mwisho katika sura hii ni mstari wa 22 ambayo ni idadi ya utimilifu hapo kukiwa na erufi 22 kwa alfabeti ya Waebrania pia ni asili  ya muudo wa unabii na kumi na mbili.


22 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. (Biblia Takatifu BT)



Sura ifuatayo katika maandiko inashughulika na vipeo vya unabii na Serikali ya Mungu. Katika mstari wa kwanza maandiko yanaonyesha agizo na katika msitari wa pili itikio la utiifu katika Roho. Na tatu katika mpangilio ni kumwona Mungu  na sherikali imeelezwa katika mstari wa nne kuwa sherikali imo katika vipengee vinne na sehemu mbili ya kumi na mbili kujumuisha idadi ya wazee ishirini na wanne ambao wanazunguka kiti cha Enzi cha Mungu .Taji zinashiria utawala na mamlaka/na uwezo.



Msitari wa tano unaonyesho uwezo na kuashiria Nehema. Ni katika sehemu hii ambayo Roho za Mungu saba zimo mbele ya kiti cha enzi kama taa saba za moto. Hizi ni Roho za ufahamu za matumizi ya uwezo wa Mungu.



Ufunuo, Sura ya 4:

1 Baada ya hayo naliona, na tazama, mlango ukafunguka mbinguni, na sauti ile ya kwanza niliyoisikia kama sauti ya baragumu ikinena nami, ikisema, Panda hata huku, nami nitakuonyesha mambo ambayo hayana budi kuwako baada ya hayo. 2 Na mara nalikuwa katika Roho; na tazama, kiti cha enzi kimewekwa mbinguni na mmoja ameketi juu ya kile kiti; 3 na yeye aliyeketi alionekana mithili ya jiwe la yaspi na akiki, na upinde wa mvua ulikizunguka kile kiti cha enzi, ukionekana mithili ya zumaridi. 4 Na viti ishirini na vinne vilikizunguka kile kiti cha enzi, na juu ya vile viti naliona wazee ishirini na wanne, wameketi, wamevikwa mavazi meupe; na juu ya vichwa vyao walikuwa na taji za dhahabu. 5 Na katika kile kiti cha enzi kunatoka umeme na sauti na ngurumo. Na taa saba za moto zilikiwaka mbele ya kile kiti cha enzi, ndizo Roho saba za Mungu. (Biblia Takatifu BT)



Ni kupitia kwaRoho Saba za Mungu ambapo ubinadamu utaelimishwa na kukombolewa. Hivyo imo sita katika mpangilio na viumbe hai vine vimejumuishwa katika hao waliokombolewa kutoka dunia. Kipengee cha nane uonyesha nyadhifa zao na kusudi lao.



6 Na mbele ya kile kiti cha enzi kulikuwa namfano wa bahari ya kioo, kama bilauri; na katikati ya kile kiti cha enzi, na pande zote za kile kiti, walikuwako wenye uhai wanne, wamejaa macho mbele na nyuma. 7 Na huyo mwenye uhai wa kwanza alikuwa mfano wa simba; na mwenye uhai wa pili alikuwa mfano wa ndama; na mwenye uhai wa tatu alikuwa na uso kama uso wa mwanadamu; na mwenye uhai wa nne alikuwa mfano wa tai arukaye. 8 Na hawa wenye uhai wanne, kila mmoja alikuwa na mabawa sita; na pande zote na ndani wamejaa macho, wala hawapumziki mchana wala usiku, wakisema, Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, Bwana Mungu Mwenyezi, aliyekuwako na aliyeko na atakayekuja. (Biblia Takatifu BT)



Mistari tatu inayofuata au vingee uonyesha uongozi katika utukufu na ibada kwa Mungu kama Muumbaji na Mungu wa uumbaji.



9 Na hao wenye uhai wanapompa yeye aketiye juu ya kiti cha enzi utukufu, na heshima, na shukrani, yeye aliye hai hata milele na milele, 10 ndipo hao wazee ishirini na wanne huanguka mbele zake yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi, nao humsujudia yeye aliye hai hata milele na milele, nao huzitupa taji zao mbele ya kile kiti cha enzi, wakisema, 11 Umestahili wewe, Bwana wetu na Mungu wetu, kuupokea utukufu na heshima na uweza; kwa kuwa wewe ndiwe uliyeviumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako, navyo vikaumbwa. (Biblia Takatifu BT)



Sehemu hii imo katika vipengee kumi na moja na kwamba kumi na moja ni kiwango fulani nusu ya ukamilifu na ni katika kiwango hiki tunapata watakatifu (Elohimu) wawili waliohitimu kutawala. Lakini hakuna wakuwakomboa katika mauti; na jeshi alihitaji mmoja wao kuwakomboa wote kutokana na maasi. Mpango wa Mungu ungetimika bali hapakuwa na yeyote aliyestahili.



Ufunuo, Sura ya 5:

1 Kisha nikaona katika mkono wa kuume wake yeye aliyeketi juu ya kile kiti cha enzi kitabu kilichoandikwa ndani na nyuma, kimetiwa muhuri saba. 2 Nikaona malaika mwenye nguvu akihubiri kwa sauti kuu, N'nani astahiliye kukifungua kitabu, na kuzivunja muhuri zake? 3 Wala hapakuwa na mtu mbinguni, wala juu ya nchi, wala chini ya nchi, aliyeweza kukifungua hicho kitabu, wala kukitazama. 4 Nami nikalia sana kwa kuwa hapakuonekana mtu astahiliye kukifungua hicho kitabu, wala kukitazama. (Biblia Takatifu BT)



Katika sehemu nneza kwanza mwaliko wa ustahilifu umetajwa kwa haraka na hapakuwa na yeyote aliyestahili. Sehemu ya tano na juu ya Rehema tena ambapo simba wa Yunda na mzizi wa uzao wa Daudi alipata ustahili.



5 Na mmojawapo wawale wazee akaniambia, Usilie; tazama, Simba aliye wa kabila ya Yuda, Shina la Daudi, yeye ameshinda apate kukifungua kile kitabu, na zile muhuri zake saba. (Bilblia Takatifu BT)



Katika kipengee cha sita tunaona mwanakondoo akichinjwa yule ambaye alikuwa amesimama kati ya Mungu na viumbe hai vinne kuashiria mamlaka juu ya uumbaji wote tendaji kwa Mungu. Alikuwa na pembe saba ambazo ni idadi ya makanisa kuashiria utawala wa wateule kama wafalme na wakuhani. Macho saba hizo ni Roho Saba za Mungu ambazo kwazo utibithi na kushauri uumbaji na wateule wa Mungu.



6 Nikaona katikati ya kile kiti cha enzi nawale wenye uhai wanne, na katikati ya wale wazee, Mwana-Kondoo amesimama, alikuwa kana kwamba amechinjwa, mwenye pembe saba na macho saba, ambazo ni Roho saba za Mungu zilizotumwa katika dunia yote. (Biblia Takatifu BT)



Mpangilio wa saba uonyesha utimisho wa kazi ya muhimu na kupokea mamlaka na uwezo juu ya mpango wa Mungu. Wa nane katika mpangilio uonyesha mwanzoni wa utawala wake na uwezo alioupokea kutoka kwa mkono wa kulia wa Mungu.



7 Akaja, akakitwaa kile kitabu katika mkono wakuume wake yeye aliyeketi juu ya kile kiti cha enzi. 8 Hata alipokitwaa kile kitabu, hao wenye uhai wanne na wale wazee ishirini na wanne wakaanguka mbele za Mwana-Kondoo, kila mmoja wao ana kinubi, na vitasa vya dhahabu vilivyojaa manukato, ambayo ni maombi ya watakatifu. (Biblia Takatifu BT)



Kutoka kwampangilio wa tisa baada ya Kristo alikuwa amekamilisha kazi yake na akahitimu kutawala wateule wa jeshi wakipokezwa wimbo mpya. Wamekubalika kuwa wakombolewa na watatawala katika dunia kama wafalme na Makuhani. Mpangilio huu ni tatu mara tatu na kwake wenyewe unayo umuhimu wa ukamilifu katika Roho mtakatifu.



9 Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake; kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa, 10 ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu; nao wanamiliki juu ya nchi. 11 Nikaona nikasikia sauti ya malaika wengi pande zote za kile kiti cha enzi, na za wale wenye uhai, na za wale wazee, na hesabu yao ilikuwa elfu kumi mara elfu kumi na elfu mara elfu, 12 wakisema kwa sauti kuu, Astahili Mwana-Kondoo aliyechinjwa, kuupokea uweza na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu na baraka. (Biblia Takatifu BT)



Msitari wa kumi na mbili umekamilisha sehemu fulani katika uhitimu na uwezo wa mwanakondoo.



13 Na kila kiumbe kilichoko mbinguni na juu ya nchi na chini ya nchi ya juu ya bahari, na vitu vyote vilivyomo ndani yake, nalivisikia, vikisema, Baraka na heshima na utukufu na uweza una yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na yeye Mwana-Kondoo, hata milele na milele. 14 Na wale wenye uhai wanne wakasema, Amina. Na wale wazee wakaanguka, wakasujudu. (Biblia Takatifu BT)



Mistari ya kumi na tatu na kumi na nne uonyesha ukamilisho wa utukufu wa Mungu na Mwanakondoo aliyetukomboa na aliyepokea uwezo na mamlaka kutoka kwa Mungu Baba yake ambaye ni Mungu wa Baba yetu pia.



Mwanakondoo hapo amefungua mihuri saba na haya yanaelezewa katika masomo haya.




Migawanyiko hii saba ya maandiko uelezea  kwa kina mpango wa Mungu chini ya Roho Saba za Mungu.



Ufunuo sura ya 8 nimtengo wa nane katika utimilifu wa mpango wa Mungu chini ya mamlaka ya Kristo. Inahusu muhuri wa saba na wakati huo umefunuliwa maombi ya watakatifu yanamiminiwa juu ya madhabahu ya Mungu. Wazee ishirini na wanne walikuwa na jukumu kwa ajili ya hayo maombi. Malaika saba wa makanisa saba hapo watapewa mamlaka na tarubeta za uwezo wa Mungu kutoa notisi na kuangamiza.



Ufunuo, Sura 8:

1 Hata alipoifungua muhuri ya saba, kukawa kimya mbinguni kama muda wa nusu saa. 2 Nami nikawaona wale malaika saba wasimamaombele za Mungu, nao wakapewa baragumu saba. 3 Na malaika mwingine akaja akasimama mbele ya madhabahu, mwenye chetezo cha dhahabu, akapewa uvumba mwingi, ili autie pamoja na maombi ya watakatifu wote juu ya madhabahu ya dhahabu, iliyo mbele ya kiti cha enzi. 4 Na moshi wa ule uvumba ukapanda mbele za Mungu pamoja na maombi ya watakatifu, kutoka mkononi mwa malaika. (Biblia Takatifu BT)



Mistari minne katika sura hii ushughulika na kuhamishwa kwa uwezo kwenda kwa wateule na malaika wa Kanisa saba za Mungu.



Maombi ya watakatifu yanatimishwa na Roho Saba za Mungu na wateule wa watakatifu waanza kuhukumu dunia na kuitawala.



5 Na huyo malaika akakitwaa kile chetezo, akakijaza moto wa madhabahu, akautupa juu ya nchi, kukawa radi na sauti na umeme na tetemeko la nchi.(Biblia Takatifu BT)



Mstari wa sita ni wa tendo bali wakati huu tendo la binadamu liko chini ya uwezo wa jeshi isipokuwa hile ya binadamu utenda kazi peke yake huku ikifuatiwa na shetani na iliyokatishwa kutoka kwa Mungu.



6 Na wale malaika saba wenye baragumu saba wakajifanya tayari ili wazipige. (Biblia Takatifu BT)



Mstari wa saba umeanza mchakato wa muhuri wa saba na tarumbeta ya kwanza ilianza ambayo ndiye anayeingilia maombi ya watakatifu.



7 Malaika wa kwanza akapiga baragumu, kukawa mvua ya mawe na moto vilivyotangamana na damu, vikatupwa juu ya nchi; theluthi ya nchi ikateketea, na theluthi ya miti ikateketea, na majani mabichi yote yakateketea. 8 Malaika wapili akapiga baragumu, na kitu, mfano wa mlima mkubwa uwakao moto, kikatupwa katika bahari; theluthi ya bahari ikawa damu. 9 Wakafa theluthi ya viumbe vilivyomo baharini, vyenye uhai; theluthi ya merikebu zikaharibiwa. 10 Malaika wa tatu akapiga baragumu, nyota kubwa ikaanguka kutoka mbinguni, iliyokuwa ikiwaka kama taa, ikaanguka juu ya theluthi ya mito, na juu ya chemchemi za maji. 11 Na jina lake ile nyota yaitwa Pakanga; theluthi ya maji ikawa pakanga, na wanadamu wengi wakafa kwa maji hayo, kwa kuwa yalitiwa uchungu. 12 Malaika wa nne akapiga baragumu, theluthi ya jua ikapigwa, na theluthi ya mwezi, na theluthi ya nyota, ili kwamba ile theluthi itiwe giza, mchana usiangaze theluthi yake, wala usiku vivyo hivyo. 13 Kisha nikaona, nikasikia tai mmoja akiruka katikati ya mbingu, akisema kwa sauti kuu, Ole, ole, ole wao wakaao juu ya nchi! Kwa sababu ya sauti zisaliazo za baragumu za malaika watatu, walio tayari kupiga. (Biblia Takatifu BT)



Mistari sabainafuata muundo wa nne wa mistari nne ya kwanza ya tarubeta saba. Ambapo tunaona kuanguka kwa serikali ya ulimwengu bali katika mpangilio ulioratibigwa.



Maandiko yanaendelea kushughulika na vipeo vya utawala bali hiyo imezungumziwa katika masomo haya Mihuri Saba [140]na Baragumu Saba [141]ilivyo arifiwa hapo juu.



Milio saba



Hata baada ya malaika kupuliza taabu zimekwisha na theluthi ya ubinadamu wameuawa (Vile tunaona katika Ufunuo sura 9), watu wa dunia hawakutubu.



Ufunuo 9:1

1 Malaika wa tano akapiga baragumu, nikaona nyota iliyotoka mbinguni, imeanguka juu ya nchi; naye akapewa ufunguo wa shimo la kuzimu. 2 Akalifungua shimo la kuzimu; moshi ukapanda kutoka mle shimoni kamamoshi wa tanuru kubwa; jua na anga vikatiwa giza kwa sababu ya ule moshi wa shimoni. 3 Nzige wakatoka katika ule moshi, wakaenda juu ya nchi, wakapewa nguvu kama nguvu waliyo nayo nge wa nchi. 4 Wakaambiwa wasiyadhuru majani ya nchi, wala kitu cho chote kilicho kibichi, wala mti wo wote, ila wale watu wasio na muhuri ya Mungu katika vipaji vya nyuso zao.(Biblia Takatifu BT)



Malaika wa Mungu, akisimama katika bahari, aliinua mkono wake na akaapa kwake anayesimama milele, aliye ziumba mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo, akisema hakuna muda mwingine kamwe (10:6).



Imajulikana kwamba Katika wakati wa kutolewa kwa mlio wa malaika wa saba, siri ya Mungu ilifunuliwa jinsi ilifunuliwa kupitia kwa watumishi wak amnao ni manabii, utamatatimzwa.



Roho hizi saba za Mungu zilinenabali siri ilikuwa tayari imefunuliwa kwa Daudi miaka elfu moja kabla lakini matumizi yake haikuwa kana kwamba yatafunuliwa. Tunapata matumishi katika Zaburi 28 na 29.



Zaburi 28

Zaburi ya Daudi

1 Ee Bwana, nitakuita Wewe, mwamba wangu, Usiwe kwangu kama kiziwi. Nisije nikafanana nao washukao shimoni, Ikiwa umeninyamalia. 2 Uisikie sauti ya dua yangu nikuombapo, Nikipainulia patakatifu pako mikono yangu.
3 Usinikokote pamoja na wasio haki, Wala pamoja na watenda maovu. Wawaambiao jirani zao maneno ya amani, Lakini mioyoni mwao mna madhara. 4 Uwape sawasawa na vitendo vyao, Na kwa kadiri ya ubaya wa kufanya kwao, Uwape sawasawa na kazi ya mikono yao, Uwalipe stahili zao. 5 Maana hawazifahamu kazi za Bwana, Wala matendo ya mikono yake. Atawavunja wala hatawajenga; 6 Na ahimidiwe Bwana. Maana ameisikia sauti ya dua yangu; 7 Bwana ni nguvu zangu na ngao yangu. Moyo wangu umemtumaini, Nami nimesaidiwa; Basi, moyo wangu unashangilia, Na kwa wimbo wangu nitamshukuru. 8 Bwana ni nguvu za watu wake, Naye ni ngome ya wokovu kwa masihi wake. 9 Uwaokoe watu wako, uubariki urithi wako, Uwachunge, uwachukue milele.(Biblia Takatifu BT)



Zaburi ni kusihi Mungu hili kuuwaokoa watu wake kama kimbilio la wenye upako wake. Msitari wa tano ni tetesi la kusihi Rehema za Mungu kuingilia kati. Mstari wa sita hausiani na vitendo vya wanadamu bali ni baraka za kusujudu Bwana kwa kuwa asikia maombi ya wanadamu. Hivyo ni katika mfano wa namna hii ambako vitendo vya wanadamu vilitanguliza vitendo vya wokovu vya Mungu.



Mstari wa saba umetamatika kwa kumsujudu Bwana kama uweza na ngao ya walio na upako ambao ni wateule watakatifu wakiwa kama nyumba ya Daudi chini ya malaika wa Bwana akiwa kwenye vichwa vyao. (C.F Zakaria  12:8). Msitari wa nane umeweka  Yehovakama uwezo wa waliopokea upako. Hii ni kicho cha moja kwa moja kwake Kristo kwa jinsi Masihi anarejea kuwakomboa walio na upako. Hali hilio katika Zaburi utambua hili kwa idadi hilyo kwenye mpangilio wa nane.



Msitari wa 9 ni tetesi la moja kwa moja kwake Masihi ili “waokoe watu wako na kubariki urithi wako walize pia na uwainue juu milele”.



Urithi wa Yehova ni nyumba yote ya Israeli, ambayo kiroho ni mwili wa kiroho wa Kanisa.



Hii basi inayo uhusiano kwa Zaburi  zinazofuata  ambazo ni urejeleo wa milio saba.



Zaburi 29:

 Zaburi ya Daudi

1 Mpeni Bwana, enyi wana wa Mungu, Mpeni     Bwana utukufu na nguvu; 2 Mpeni Bwana utukufu wa jina lake; Mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu. 3 Sauti ya Bwana i juu ya maji; Mungu wa utukufu alipiga radi; Bwana yu juu ya maji mengi. 4 Sauti ya Bwana ina nguvu; Sauti ya Bwana ina adhama; 5 Sauti ya Bwana yaivunja mierezi; Naam, Bwana aivunja-vunja mierezi ya Lebanoni; 6 Airusha-rusha kama ndama wa ng'ombe; Lebanoni na Sirioni kama mwana-nyati. 7 Sauti ya Bwana yaipasua miali ya moto; 8 Sauti ya Bwana yalitetemesha jangwa; Bwana alitetemesha jangwa la Kadeshi. 9 Sauti ya Bwana yawazalisha ayala, Na kuifichua misitu; Na ndani ya hekalu lake Wanasema wote, Utukufu. 10 Bwana aliketi juu ya Gharika; Naam, Bwana ameketi hali ya mfalme milele. 11 Bwana atawapa watu wake nguvu; Bwana atawabariki watu wake kwa amani. (Biblia Takatifu BT)



Mandishi unena katika msitari wa 1:

1Mpeni Bwana, enyi wana wa Mungu”; Walakini Targumi utolea malaika na ni wazi kwamba hapa tunashughulika na watakatifu (Elohim).



Wana wa Mungu wanawajibika kwa kutoa tukufu wao na uwezo wao kwa Yehova. Utukufu kwa ajili ya Yehova upo katika ibada kwenye uzuri wa utakatifu.



Zaburi ni jibu la kusihi kwenye Zaburi 28 na hasa katika baadhi ya Zaburi 28:7-8.



Mstari wa 3 hapo unanena: “Sauti ya Bwana i juu ya maji; Mungu wa utukufu alipiga radi”.



Hivyo tunashughulika nasauti ya Bwana ambaye ni Utukufu wa Mungu unaopiga radi. Huyu kiumbe ni Yahova wa Zaburi 45:6-7 aliyekuwa na Israeli pale jangwani na ambaye anatambulika kama Masihi katika Waebrania 1:8-9.



Katika maandiko haya tunaona kwamba Neno  sauti ya Bwana limetumika mara saba. Hii inatuelezea mjengo ambayo kwayo milio sabailipulizwa. Ilikuwa majibu ya moja kwa moja kwa ajili ya mshahada katika Zaburi 28 hapo awali.



Utumika kuashiria kurejea kwa Masihi hili kuokoa wale ambao wanamngoja kwa thati katika siku za mwisho.



Sauti ya Bwana itaguza maji mengi ndio kusema watu wengi wa mataifa.



Katika mlio wa pili, Bwana atakabili mataifa yale katika nguvu na uwezo kwa jinsi walivyo wakabili wateule ilivyotajua katika fumbo  la kondoo na mbuzi.



Mlio wa tatu utaasisi utukufu wa Yahova juu ya ulimwengu katika kutiisha. Neno ni hadar (SHD 1926, utamkwa hawdawr), ambaye umaanisha utukufu.



Zaburi 29:5 inasema sauti ya Bwana ambayo ni mlio wa nne, umevunja mierezi za Lebanoni. Lebanoni na Sirioni, au Herimoni uruka kama ndama ya ndume wa mwituni.



Ndio kusema, Mungu upiga mashariki ya kati na mtetemeko mkuu wa ardhi.



Sauti kama mlio wa tano hugawa miale ya  moto. Sehemu hii, kama msitari wa saba , unaambatana na miale ya moto. Hili kutumia nguvu za asili kukabiliana na uwezo wa kidunia.



Sauti kama mlio wa sita utetemesha ulimwengu na ulimwengu wa kadeshi ndio hasa umetajua .Hata hivyo, haujafunganishwa kwa Kadeshi tuu.



Sauti ya Bwana kamamlio wa saba ufanya minyama kupenyeza kwa kishindo na kuangamiza au kuharibu kabisa misitu yote kama matokeo ya ghahabu.



Mwishoni mwa machafuko haya wateule wataokolewa na ni ndani ya Hekalu lake, jinsi tunavyoona toka msitari wa 9, ambao unafanana na maneno ya awali katika msitari wa 9 wa Zaburi 28.



Zaburi 29:10 usema kwamba Bwana amekaa juu ya maji mengi naye ni Mfalme milele.



Maandiko haya ni sawasawa na vitendo vilivyo katika kitabu cha Mwanzo na urejelea katika msitari wa 3 wa Zaburi na Mwanzo 6:17; 7:6,7, 10,17;  9:11,15,28;  10:1,32;  11:10.



Baadhi katika kumi namoja inasema Mungu atawapa uwezo watu wake na Mungu kwa amani atawabariki watu wake.



Andiko hili liko kwenye mistari 11 sababu utendaji ujakamilika na unaendelea hadi wakati wa miaka elfu moja.



Zaburi 30 inaendelea kumuhimidi Bwana sababu ya kuingilia kati kwake na imekamilika katika mistari 12.



Katika yote, kuna Amina sabakatika Zaburi, ambayo ina uhusiano pia kwa Roho Saba za Mungu. Hayo ni masomo juu ya kuwa na uadilifu didhi yake (cf. Zaburi 41:13; 72:19; 89:52). Kunayo pia Amen kumi na mbili katika Kumbukumbu la torati sura ya 7 kwa ajili ya itikio la Agano.



La muhimu hapa ni kufahamu kwamba muundo wa andiko katika Ufunuo (vilevile popote katika  Biblia) kunayo uhalisi wake wa kiroho na umeenea katika sura ishirini na mbili kushughulikia uwezo na kutimia kwa Roho saba za Mungu ukitenda katika sambamba na Kristo kwa kukomboa Kanisa kama wateule wa Mungu, na kutwaa madaraka ya sayari katika siku za mwisho. Ufunuo ni maandiko matakatifu na maandiko matakatifu hayakuvujwa.



Roho saba za Mungu utuwezesha sisi wote kama Kanisa la Mungu kukabili Sayari hii katika siku za mwisho. Vyote pamoja ni uwenzo wa Roho Mtakatifu na ndio njia  ambazo kwazo tuafanyika kuwa watakatifu wa mbinguni au Elohim.





MUNGU AKUBARIKI SANA KARIBU SANA KATIKA BLOG HII

Post a Comment

0 Comments